Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai 28, 2017

OKWI NDANI YA AFRIKA KUSINI

Picha
Mshambuliaji Emmanuel Okwi, ametua katika kambi ya Simba nchini Afrika Kusini na leo asubuhi ameanza mazoezi. Okwi ameanza mazoezi na wenzake katika kambi ya timu hiyo jijini Johannesburg, Afrika Kusini.

MSUVA RASMI HASSANI EL JADIDI YA MOROCCO

Picha
Kiungo mshambuliaji wa Tanzania Simon Msuva ametambulishwa rasmi na klabu yake mpya Difaa Hassani El Jadidi ya Morocco baada ya kusaini mkataba wa miaka mitatu kuitumikia klabu hiyo. Msuva aliondoka Dar es Salaam Julai 26, 2017 kwenda Morocco ambako atakuwa na mtanzania mwingine Ramadhani Singano ‘Messi’ ambaye yeye alifika Morocco mapema kuliko Msuva aliyekuwa na majukumu kwenye timu ya taifa.

KICHUYA AHOFIA NAMBA

Picha
wakati club ya simba ikiendelea na maanadaliazi ya mchezo wa ngao ya hisani dhidi ya mahasimu zao yanga pamoja na maanadalizi ya msimu ujao uko Afrika kusini. mshambuliaji wa simba Shiza kichuya amefunguka na kusema anahisi msimu ujao itakuwa mgumu kwake kutokana na usajir mpya ndani ya kikosi chao na ujio wa emmanuel Okwi kichuya anayecheza wingi ya kulia na kushoto amesema kwa sasa simba inawachezaji wa kutosha wa kunyakua makombe na kutesa kimataifa pia kichuya anamsubiri kwa hamu okwi na niyonzima kwani anahamu ya kucheza nao kikosi cja kwanza japo anamuachia kocha ndo anajuwa nani acheze hapa au nani amalize hapa kichuya     

FLOYD MAYWEATHER TENA ULINGONI KUMUONA $150000

Picha
Tiketi za kushuhudia mpambano wa masumbwi kati ya Floyd Mayweather dhidi ya Conor McGregor zinauzwa kwa dola 150,000. Mpambano huo unatajwa kuwa wa gharama zaidi kuwahi kutokea na tiketi kwa sasa zinauzwa kama njugu. Unatarajiwa kupigwa Agosti 26 katika uwanja wa T-Mobile mjini Las Vegas utakaoingiza watu elfu 20. Mayweather mwenye miaka 40 awali alistaafu lakini amerejea kupambana na McGregor.

KITASA CHA SIMBA SPORT CLUB CHANUKIA ORLANDO PIRATES

Picha
Kampala, Uganda. Orlando Pirates ipo tayari kumnunua beki wa Uganda, Simba SC, Murushid Juuko kwa mujibu wa KickOff.com. Beki huyo wa Uganda, Juuko ameripotiwa kuwa yuko njiani kujiuanga na miamba hiyo ya Soweto, Orlando Pirates. Beki huyo mwenye miaka 23, kwa sasa yupo na kikosi cha Simba kinachojiandaa Afrika Kusini alikuwa miongoni mwa wachezaji wa Uganda Cranes walioshiriki katika Kombe la Mataifa ya Afrika 2017 nchini Gabon. Kwa mujibu wa vyanzo vya kuhaminika kutoka Uganda, Juuko alisema amekuwa akifuatiliwa na Buccaneers, ambaye wanatakiwa kununua mkataba wake wa miezi minne uliobaki na Simba. "Murushid Juuko amehusishwa na kutakiwa na Orlando Pirates,” chanzo hicho kimeimbia KickOff.com. “Ni beki mzuri anayecheza katika klabu ya Simba SC." Aliendelea kuwa: "Juuko amebakiza miezi minne katika mkataba wake wa sasa. Hivyo ni bora Simba wakakubali kuuza sasa au la kumwacha ondoke bure.”

WAZIRI JUNIOR AWAZA KUWA MFUNGAJI BORA

Picha
Mshambuliaji mpya wa Azam, Waziri Junior amesema lengo lake ni kuwa mfungaji bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu. Azam inayoendelea na maandalizi kuelekea msimu huo mpya itafungua dimba Agosti 26 kwa kucheza ugenini kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona dhidi ya wenyeji wao, Ndanda. "Inawezekana kuwa mfungaji bora wa Ligi kikubwa ni kupigania nafasi ya kuwa nacheza katika kikosi cha kwanza, changamoto ya namba ipo popote pale ila kikubwa ni kujituma. "Nimeanza kwa kufunga katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Lipuli, nafurahi kwa sababu nimekuwa na maelewano na wenzangu kwa muda mfupi." alisema. Waziri amesajiliwa na Azam akitokea Toto Africans ya Mwanza iliyoshuka daraja ili kuzipa pengo la John Bocco aliyejiunga na Simba.

DAUDA SHAFFIH AFUNGUKA KUJIENGUA KWAKE

Picha
Shaffih  Dauda anasema!! ➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖ "Unapofanya jambo lazima uangalie mwisho wake kuna manufaa gani? Nimeamua kwa maslahi mapana ya mchezo wa soka na kulinda heshima ya jina langu  kwa nia njema nimeamua kujiuzulu kugombea nafasi ya ujumbe kamati ya utendaji TFF." "Nitaendelea kushirikiana na Viongozi wa Soka kama hapo awali, kushauri na kutoa maoni yangu kama mdau katika kukuza na kuendeleza mpira wa miguu Tanzania"   "Kuonyesha uwajibikaji ni jambo Jema! Nipo kwenye mfumo wa Mpira  muda mrefu naijua mizengwe na fitna kuna watu nyuma yangu wanaonitizama ukichafuliwa kwa Rushwa ni kuharibu future yako."

SPORTPESA YAVAMIA UGANDA

Picha
ile kampuni nguri ya udhamini imevamia nchini uganda baada ya kuvamia katika ligi ya Tanzania bara na visiwani katika baadhi ya timu kama vile simba yanga na singida hizo ni baadhi ya yimu tu zilizovamiwa na kuvuna mapesa ya sportpesa rais Yower Mseveni akionesha huodari wake wa kuchezea mpira mchini uganda alipotembelewa na sportpesa

TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

Picha
TETESI ZA SOKA ULAYA IJUMAA 28.07.2017 Arsenal wanakaribia kukamilisha usajili wa pauni milioni 45 kumchukua kiungo wa Monaco Thomas Lemar, 21. (Sun) Monaco wamekataa dau la tatu la Arsenal la pauni milioni 44.7 la kumtaka Thomas Lemar. (L’Equipe) Meneja wa Real Madrid Zinedine Zidane amesema hawezi kutoa hakikisho kuwa Gareth Bale atabakia Bernabeu msimu huu, huku Manchester United wakimfuatilia. (Mirror) Monaco watakuwa tayari kumuuza Kylian Mbappe kwa timu itakayokuwa tayari kutoa euro milioni 180. (L’Equipe) Meneja wa Chelsea Antonio Conte anapanga kutoa pauni milioni 50 kuwasajili Ross Barkley, 23, kutoka Everton na Alex Oxlade-Chamberlain, 23, kutoka Arsenal. (Sun) Chelsea wamepanda dau kutaka kumsajili kwa mkopo Renato Sanches, 19, kutoka Bayern Munich. (Daily Telegraph) Meneja wa Tottenham Mauricio Pochetitino anataka kumsajili Ross Barkley na kumfanya kuwa kiungo wa kati. (Times) Roma wanajiandaa kupanda dau jipya la pauni milioni 32 kumtaka winga wa kimatai...

SHAFFIH DAUDA AKIMBIA SIASA CHAFU DHIDI YAKE

Picha
Mkuu wa Vipindi wa Cloudsfm ambaye pia ni mdau mkubwa wa mpira wa Miguu, Shaffih Dauda ametangaza kujitoa rasmi kwenye mchakato wa uchaguzi wa TFF. @shaffih amesema amefikia hatua hiyo baada ya kuona mbinu na siasa chafu zinazoendeshwa dhidi yake. " Mimi ni mfanyakazi wa CloudsMediaGroup, nilikwenda Mwanza kwa ajili ya kazi. Hapa Clouds tumelelewa kufanya kazi kwa bidii kufikia malengo na sitaki mambo yangu binafsi ( kugombea uongozi TFF ) kuharibu malengo ya NdondoCup na Taasisi kwa ujumla. Pia nimehangaika kutengeneza jina langu kwa miaka mingi. Natangaza kujitoa rasmi, na nitaendelea kuchangia kwenye maendeleo ya soka nchi hii nikiwa sio kiongozi " @shaffih.

MBEYA CITY KAMA SIMBA VILE

Picha
KAMA unaishangaa Simba kusajili kikosi kizima na wachezaji wa akiba juu, Mbeya City nayo inapita mulemule ambapo jana Alhamisi ilitangaza majina 23 ya wachezaji ambao watakuwa nao msimu ujao ba bado wakisisitiza kuwa bado watasajili wachezaji wengine watano wapya. Zikiwa zimebaki siku 10 kabla ya dirisha la usajili kufungwa, Kaimu Ofisa Habari wa Mbeya City, Shaa Mjanja, alisema kuwa licha ya timu hiyo kufanya usajili wa wachezaji zaidi ya watano wapya, bado hawajafunga zoezi hilo na kabla ya wiki hii kumalizika watawatambulisha wachezaji wengine. Shaa alisema kikosi kipo kambini, lakini kutokana na ripoti ambayo ilipendekezwa na benchi la ufundi wanatakiwa kusajili wachezaji wengine watano ili kuwa tayari kwa mapambano ya msimu ujao. Wachezaji hao ni, Fikirini Bakari, Majaliwa Shabani, Hassan Mwasapile, Hamisi Msabira, Ally Lundenga, Erick Kiaruzi, Babu Ally, Issa Selemani, Rajabu Isihaka, John Kabanda, Danny Joram, Frank Hamisi, Sankan Mkandawile, Owen Chaima, Mrisho Ngassa, Medso...

TAKUKURU YALA SAHANI MOJA NA TFF

Picha
Mwanza. Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru)Mkoa wa Mwanza imesema inaendelea kufanya uchunguzi dhidi ya baadhi ya wagombea na wapiga kura katika Shirikisho la Soka nchini (TFF) waliokamatwa jijini Mwanza wakibainika na makosa watapelekwa mahakamani. Juzi Jumanne Takukuru iliwatia nguvuni jumla ya watu 10 wakiwamo wagombea wa nafasi za kamati tendaji TFF kwa madai ya kufanya kampeni kabla ya muda wake na kuwapo kwa viashiria vya utoaji rushwa, ambapo watuhumiwa waliachiwa kwa dhamana. Mkurugenzi wa Takukuru mkoani Mwanza, Ernest Makale amesema uchunguzi unaendelea na kwamba wakipata ushahidi rasmi watawapeleka mahakamani. "Bado tunazidi kufanya uchunguzi na ushahidi ukipatikana watuhumiwa watapandishwa mahakamani, tuliwaachia kwa dhamana," amesema Makale. Ameongeza kuwa uchunguzi huo wanatarajia kuufanya haraka ili kabla ya uchaguzi mkuu wa TFF kufanyika, Agosti 12 wawe wameshakamilisha. "Tunajua uchaguzi ni Agosti 12, sisi Takukuru tutahakikisha kabl...

MWANJALI AMUWAHI IBRAHIMU AJIBU

Picha
MASHABIKI wa Yanga wanachonga sana mitaani kwa sasa kutokana na majembe ya maana yaliyotua kikosini mwao akiwamo Ibrahim Ajibu aliyeungana na akina Donald Ngoma, Obrey Chirwa na Amissi Tambwe kuipa makali safu yao ya mbele. Lakini kama Yanga inatarajia mteremko katika pambano la Ngao ya Jamii dhidi ya Simba litakalopigwa Agosti 23 Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, pole yao. Habari ni kwamba yule beki kisiki Mzimbabwe Method Mwanjali karudi mapema. Mwanjali aliyekuwa majeruhi kwa muda mrefu Simba, amepona na ameanza mazoezi sambamba na nyota wenzake waliopo kambini Afrika Kusini. Kama hujui, Mwanjali ndiye aliyechangia kwa kiasi kikubwa kuinyima Yanga mabao katika pambano la duru la kwanza la Ligi Kuu Bara msimu uliopita lililochezwa Oktoba Mosi, 2016 na kumalizika kwa sare ya bao 1-1. Katika pambano hilo, Yanga ilipata bao lake la utatanishi lililofungwa kwa kutengenezwa na mkono na straika wake, Amissi Tambwe kabla ya Shiza Kichuya kuisawazishia Simba bao la kideoni kwa mpira...

MNAGERIA WA YANGA AANZA VITAMBO

Picha
S HIZA Kichuya alijipatia umaarufu mkubwa msimu uliopita kwa bao lake la kideoni alilomtungua kipa Ally Mustafa ‘Barthez’ na kuisawazishia Simba bao katika pambano dhidi ya Yanga, lakini sasa Simba lazima wake chonjo. Yanga imeleta beki shupavu wa kati kutoka Nigeria ambaye zinahesabiwa siku kabla ya kumwaga wino. Jamaa ni mbaya kwa mipira iliyokufa na fundi wa kutupia kambani mipira iliyochongwa kona, huku akiwa na sifa ya kupiga kwa miguu yote miwili. Beki huyo ni Henry Tony Okoh anayewania nafasi moja ya nyota wa kigeni iliyosalia Yanga sambamba na kiungo Mkameruni, Fernando Bongyang. Jamaa huyo bwana, kwa mipira ya mguu wa kushoto ni mzuri, huko kulia ndio usiseme na kama Yanga itamsainisha mkataba wa kuitumikia timu hiyo ni vema nyota wa Simba na timu nyingine za Ligi Kuu Bara wasijaribu kabisa kutoa mipira ya kona. Mwanaspoti limefanya mazungumzo na beki huyo na kufunguka mambo mengi ikiwamo umahiri wake wa mipira iliyokufa na kufunga kwa vichwa. ALIVYOIJUA YANGA ...

TAHARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Picha
Klabu ya Simba kwa masikitiko makubwa inakanusha taarifa potofu zinazosambaa mitandaoni na kwenye baadhi ya vyombo vya habari,kuwa imecheza mechi ya kirafiki nchini Afrika kusini,na kupoteza mchezo huo. Uzushi huo unasema Simba imefungwa mchezo huo kwa jumla ya goli 7-0, na timu ya daraja la kwanza ya nchini humo, Royal Eagles. Kiukweli Simba haina rekodi za hovyo kama hizo kokote inapocheza duniani,na haijawahi kufungwa na klabu yoyote idadi ya magoli kama hayo,kama zilivyo klabu nyingine nchini,hususan klabu ambayo mashabiki wake ndio wanaozusha upuuzi huo. Dunia ya leo ni ya Teknolojia, na ingekuwa ni kweli,hakuna mtanzania ambae asingeiona hii taarifa kutoka kwenye mitandao au vyombo vya habari vya Afrika kusini. Tunapenda Umma wa watanzania utambue kwa siku zote tulizokuwa huko,program ya benchi la ufundi, ilijikita ktk kuitengeneza miili ya wachezaji kistamina. Wiki ijayo Timu yetu inatarajiwa kucheza mechi mbili na klabu za Orlando Pirates na Bidverst za nchini humo, kabla ...