Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti 11, 2017

MAGAZETI LA LEO JUMAMOSI

Picha

MKUTANO SIMBA UPO PALEPALE

Picha
SIMBA SPORTS ​ ​ DAR ES SALAAM ​ ​ 11-8-2017 ​            ​ TAARIFA KWA UMMA ​ ​ _______________________________ ​ Klabu ya Simba inawatangazia Wanachama wake na wadau wa mchezo wa kandanda kote nchini kuwa Mkutano wake mkuu wa kawaida wa kila mwaka upo pale pale. Hatua hiyo inafuatia na Hukumu iliyosomwa leo katika Mahakama ya kisutu, kufuatia zuio la kuzuia Mkutano huo, liliowekwa na mmoja wa wadhamini wa klabu Mzee Hamis kilomoni. Kwenye hukumu hiyo,mahakama hiyo ilitupilia mbali shauri hilo. Mkutano huo utafanyika siku ya Jumapili tarehe 13-8-2017, kuanzia saa Nne kamili asubuhi, ukitanguliwa kwa Wanachama wa klabu kujiandikisha kuanzia saa mbili kamili asubuhi. Klabu imeamua kufanyia mkutano huo kwenye Ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (Mwalimu Nyarere international Conference Centre). Ukumbi huo wa kisasa kabisa nchini upo maeneo ya Ocean Road, jirani na Chuo c...

WATOTO WA WENGER WAFUNGUA LIGI KUU ENGLAND

Picha
Watoto wa Wenger kufungua dimba la EPL Utamu wa Ligi Kuu ya England unarejea kuanzia leo ambapo watoto wa mzee Wenger, Timu ya Arsenal itafungua dimba hilo kwa kuoneshana ubabe na Leicester City. Kuelekea mchezo huo unaopigwa Emirates, Arsenal imejiweka sawa kuendeleza rekodi yake ya kuinyanyasa Leicester City katika ligi hiyo, huku ikitafuta nafasi ya kurekebisha makosa katika mechi za fungua dimba ambapo katika mechi 7, imeshinda mechi moja pekee. Arsenal wanaingia kwenye mchezo huo wakiwa na kumbukumbu nzuri ya kutwaa ubingwa wa ngao jamii dhidi ya mabingwa wa EPL Chelsea FC lakini inamkosa mshambuliaji wake tegemeo Alexis Sanchez ambaye ni majeruhi. Baada ya mechi hiyo ya ufunguzi inayopigwa saa 3:45 usiku wa leo , mechi nyingine saba zinapigwa kesho Jumamosi kama ifuatavyo:- Watford Vs Liverpool Chelsea Vs Burnley Crystal Palace Vs Huddersfield Everton Vs Stoke City Southampton Vs Swansea City West Brom Vs Bounermouth Brighton Vs Man City Ligi hiyo itaendelea tena Jum...

SHAFII DAUDA AFUNGUKA KUHUSU UCHAGUZI WA TFF DODOMA

Picha
Dodoma. Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji katika uchaguzi mkuu wa Shirikisho la soka nchini (TFF) Shafii Dauda amesema ametumia demokrasia kugombea nafasi hiyo yupo tayari kwa matokeo yoyote. Awali Dauda alitangaza kujitoa kwenye kinyang'anyiro hicho baada ya kuwepo na tuhuma zilizomuhisisha kwamba alihisiwa na vitendo vya rushwa jijini Mwanza ambapo alihojiwa na Takukuru na kuachiwa. Dauda alitangaza kujitoa kugombea nafasi hiyo kwa madai kwamba uchaguzi huo unaonekana kujaa siasa za kuharibiana na kuchafuliana majina, lakini watu wake wa Karibu walimshauri kukata rufaa ili kupigania haki yake. "Ni kweli nilijitoa ila washauri wangu baadaye walinishauri kukata rufaa na ndiyo maana nimerejea baada ya kubainika kwamba hazikuwa na ukweli wowote tuhuma hizo, natumia demokrasia ambayo ni haki ya kila mtu lakini kuchaguliwa ama kutochaguliwa inabaki kwa wapiga kura. "Unapitumia demokrasia basi siyo lazima uchaguliwe ndivyo ilivyo hata kwangu nisipochaguliwa...

SIMBA LEO WAICHINJA POLISI DSM 2-1

Picha
Kikosi cha Simba leo kimecheza mchezo mwingine wa kirafiki dhidi ya timu ya Polisi Dar es Salaam ambapo kikosi cha SImba kimeshinda kwa goli 2 - 1. Magoli ya kikosi cha Simba yamefungwa na Laudit Mavugo pamoja na Mwinyi Kazimoto