Machapisho

ARSENAL YAITIA NIASHAI CHELSEA NGAO YA JAMII

Picha
Arsenal yaitoa nishai Chelsea ngao ya jamii Arsenal wamefanikiwa kutwaa ngao ya jamii kuelekea kuanza kwa msimu mpya wa ligi kuu nchini Uingereza (EPL) kwa kuwafunga mabingwa wa ligi hiyo msimu ulipita, timu ya Chelsea. Washika mtutu hao wa London ambao ni mabingwa wa kombe la FA, (Ubingwa walioupata kwa kuwafunga hao hao Chelsea), leo wamenyakua ngao hiyo kwa mikwaju ya penati 4-1 baada ya kumaliza dakika 90 kwa sare ya goli moja kwa moja. Katika mchezo huo Chelsea walitangulia kupata bao kupitia kwa Victor Moses dakika ya 46 ya mchezo, kabla ya Sead Kolasinac kusawazisha dakika ya 82. Katika mikwaju ya penati, Arsenal walifunga penati nne kupitia kwa Walcott, Nacho, Chamberlain na Giroud na kwa upande wa Chelsea, Morata na Courtois walikosa penati zao huku Garry Cahili akifunga penati yake

GWIJI LA SOKA CAMPBELL ATUA JIJINI

Picha
Gwiji la soka Sol Campbell atua jijini 05 Aug 2017, 05:38 pm|  Mashabiki wa gwiji la Arsenal, Sol Campbell mapema leo, Jumamosi walionekana katika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), tayari kwa kumpokea mchezaji huyo aliyetikisha katika ulimwengu wa soka kwa muda mrefu. Mashabiki hao walionyesha kuwa na bashasha wakitaka kumuona mchezaji huyo aliyeiwezesha Arsenal kubeba vikombe enzi zake akiwa beki kisiki. Campbell ambaye ni raia wa Uingereza anawasili nchini huku akitarajiwa kushuhudia mechi ya Ngao ya Jamii kati ya Arsenal dhidi ya Chelsea. Campbell ambaye pia amewahi kuichezea Tottenham Hotspur ya England, katika ziara yake nchini ataendesha mafunzo kwa timu ya Magnet katika Uwanja wa Gymkhana na kutembelea timu ya Muungano kwenye Uwanja Karume “Huyu ni nyota wa pili wa zamani wa soka baada ya Leon Osman wa Everton, tunajua bado watu wanakumbuka ujio wa Everton huu ni muendelezo wa kuleta hamasa ya soka nchini

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAMOSI 05.08.2017

Picha
TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAMOSI 05.08.2017 Chelsea wameripotiwa kuwasiliana na Paris Saint-Germain kutaka kumsajili beki Serge Aurier, 24, huku kukiwa na taarifa kuwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast anakaribia kujiunga na Manchester United. (Manchester Evening News) Inter Milan wanataka kuwapiku Manchester United na Chelsea katika kumsajili beki Serge Aurier wa PSG. (Calciomercato) Meneja wa Monaco Leonardo Jardim amedokeza kuwa Kylian Mbappe, 18, anayenyatiwa na Real Madrid, Manchester City, Barcelona na Arsenal, huenda akaondoka kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Independent) Philippe Coutinho, 25, ameachwa katika kikosi cha Liverpool kitakachocheza na Athletic Bilbao siku ya Jumamosi kwa sababu ya jeraha la mgongo. Mchezaji huyo ananyatiwa na Barcelona ili kuziba nafasi ya Neymar. (Mirror) Barcelona wamewasiliana na Borussia Dortmund kuhusu mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa Ousmane Dembele, 20, ili kuchukua nafasi ya Neymar. (Daily Mail) Ousmane Dembele amesema ana...

NEYMAR KAWA MWENYEJI FASTA

Picha
NEYMAR FASTA AANZA MAZOEZI, UTAFIKIRI ALIJIUNGA MUDA MREFU NA PSG Unaweza ukadhani ni mwenyeji maana Neymar mara moja ameanza mazoezi na kikosi chake kipya cha PSG akionyesha ni mwenye furaha hasa. Neymar amejiunga na timu hiyo ya Ufaransa kwa dau kubwa la usajili linalokadiriwa kufikia pauni miloni 198 na kumfanya kuwa mchezaji ghali zaidi duniani. Neymar alionekana mwenye furaha akiwa na Wabrazil wenzake, Luca Moura na Dani Alvez.

KAULI YA KWANZA YA NEYMA JR.

Picha
Hii leo mshambuliaji mpya wa klabu ya Psg Neymar Dos Santos ametambulishwa rasmi mbele ya waandishi wa habari na huku akipewa jezi namba 10. Neymar ameongea mengi kuhusu uhamisho wake huu uliovunja rekodi ya dunia “nilihitaji changamoto mpya katika soka na moyo wangu ulikuwa ukiniambia kwamba Psg ni mahala sahihi kwangu” “Ilikuwa ni muda sahihi kwangu kuondoka Barcelona na kwenda kutafuta changamoto mpya na nimekuja hapa nikiwa tayari na hata kesho naweza kuanza kucheza” alisema Neymar. “Nina furaha sana kuvaa jezi ya Paris Saint German na kubeba jina la taifa langu pamoja na mimi, niko tayari kucheza popote kocha atakapotaka nicheze mimi nataka kucheza soka tu” “Paris Saint German ni klabu ambayo inataka kuja kuwa klabu kubwa duniani na mimi nataka kuwa sehemu ya watu ambao wataandika historia na klabu hii, sikuvutiwa na pesa kuja hapa bali mipango ya klabu hii” Kuhusu Javier Pastore aliyekubali kumpa jezi namba 10, Neymar alisema ...

SINGANO ANUKIA JANGWANI

Picha
KIUNGO mshambuliaji Ramadhan Singano ambaye alikuwa akiichezea Azam FC, Alhamisi mchana alirejea nchini akitokea Morocco alikokwenda kwa ajili ya kucheza soka la kulipwa katika timu ya Difaa Al Jadida. Akiwa Morocco kwenye mipango yake hiyo inaelezwa kuwa wakala wake amechangia kukwama kwa dili la kujiunga katika kikosi hicho na ndiyo maana amerejea Dar ambapo moja kwa moja amekutana na ofa ya kusajiliwa na Yanga. Singano aliondoka hapa nchini Julai 14, mwaka huu, alikwenda Morocco kwa makubaliano ya kusaini mkataba wa miaka mitatu katika timu hiyo, lakini alishangaa kufika huko na kutakiwa kufanya majaribio ambapo alicheza mechi sita. Mtu wa karibu wa mchezaji huyo, alisema: “Singano amerejea baada ya wakala wake anayeitwa Khalid kuwa na tamaa ya fedha kutokana na kupandisha dau na kwenda kinyume na makubaliano kitendo ambacho ile timu imekasirika. “Sisi kama watu wake wa karibu, tumemwambia arudi awahi dirisha la usajili hapa nyumbani kabla halijafungwa na kama ikitokea...

BOCCO NA OKWI WAMTOA UDENDA MZUNGU WA BIDVEST

Picha
Jo'burg, Afrika Kusini. Kocha wa mabingwa wa Ligi Kuu Afrika Kusini, Bidvest Wits FC, Gavin Hunt amesema amevutiwa na viwango vya John Bocco na Emmanuel Okwi ila kinachomtia woga ni dau. MCL Digital imetinga Bidvest na kujionea mazingira halisi ya klabu hiyo inayomilikiwa na chuo ikizungukwa na viwanja vya soka zaidi ya vitatu kila kimoja kwa ubora wake. Kocha Hunt alisema siku nyingi wanamtaka Bocco, lakini fedha yake kubwa, Azam walitupa dau ambalo tulishindwa kwenda nao sawa, sasa nilipomwona tena na Simba nimeshangaa na yuko katika ubora wa juu zaidi. "Mchezaji mwingine ni yule namba saba, Okwi ni mzuri hata leo tunatamani kuwa na mchezaji kama yeye," alisema Hunt. Akikizungumzia kikosi Simba kwa ujumla, Hunt alisema Simba ni timu nzuri na ina wachezaji wazuri na hasa katika safu yao ya ushambuliaji, Okwi na Bocco (kwa kuwataja majina) wana uelewano mazuri kwenye ushambuliaji. "Kwa sasa wako kwenye maandalizi na mazoezi magumu, miili ikifunguka watakuwa vizu...