Machapisho

SIMBA YATWAA NGAO YA JAMII KWA MATUTA

Picha
Dar es Salaam. Kipa Aishi Manura na kiungo Mohamed Ibrahimu wameiongoza Simba kutwaa ubingwa wa Ngao ya Jamii kwa kuifunga Yanga kwa penalti 5-4. Katika mchezo huo uliomalizika dakika 90 kwa timu hizo kutoka suluhu ndipo penalti zilipotumika kuamua bingwa wa mechi hiyo ya ufunguzi wa msimu mpya wa 2017-18. Kipa Manura aliyesajili na Simba akitokea Azam alithibisha ubora kwa kudaka penalti ya kwanza ya Yanga iliyopigwa na Kelvin Yondani. Wakati Mo Ibrahimu alifungia Simba penalti ya sita baada ya kiungo wa Yanga, Juma Mahadhi kuikosa penalti yake ya sita kwa kupaisha. Wafungaji wa Simba katika penalti hizo ni nahodha Method Mwanjali, Emmanuel Okwi, Haruna Niyonzima, Shiza Kichuya wakati Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ akikosa kabla ya Mo Ibrahimu kufunga penalti ya sita. Yanga ilianza penalti hizo vibaya kwa Kelvin Yondani na baadaye Juma Mahadhi kukosa huku walipopata ni nahodha Thaban Kamusoko, Pappy Tshishimbi, Ibrahimu Ajib, Donald Ngoma. Simba ilianza mechi hiyo kwa k...

KIKUKU CHA TSHISHIMBI CHAWA GUMZO

Picha
Kiungo mpya wa Yanga, Pappy Tshishimbi amezua minong’ono kwa mashabiki wa soka kutokana na kufunga cheni ‘kikuku’ katika mguu wake wa kushoto. Tshishimbi aliwaduwaza mashabiki wakati aliposhikuka kwenye basi la Yanga akiwa na wachezaji wenzake na kuingia uwanjani tayari kuivaa Simba. Kiungo huyo Mkongo alichelewa kujiunga na Yanga kutokana na matatizo yake ya kupata viza, hata kibari chake cha kuanza kuichezea Yanga kilipatikana leo asubuhi.

TUNALIAMSHA DUDE TAIFA

Picha
Ile siku iliyokua ikingojewa na wapenzi wengi wa soka la bongo hasa mashabiki wa timu kubwa mbili za hapa nchini,yaani hapa namaanisha ile Derby ya Kariakoo hatimae imewadia. Leo ni leo katika Uwanga wa taifa ambapo tutashudia vidume na vigogo wa soka nchini wakishuka dimbani kumenyana katika mchezo wa Ngao ya Hisani ikiwa ni ishara ya kufunguliwa kwa pazia la ligi kuu Vodacom Tanzania ambayo inatarajiwa kuanza kutimua vimba Jumamosi hii katika viwanja mbalimbali hapa nchini. Miamba hao wa soka nchini (Simbana Yanga) wanatarajiwa kushuku dimbani mida ya Saa 11:00 jioni ya leo kucheza mchezo huo huku presha ikizidi kuongezeka kila wakati. Wakuu wa vitengo vya habari wa timu zote wamethibitisha vikosi vyao kua imara na kua tayari kwa mtanange huo licha ya mapungufu walio nayo. Mpendwa msomaji wa vyankende.com ikumbukwe kua baadhi ya wachezaji wa Yanga hawatacheza mchezo huo kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na majeruhi na yule aliekutana na rungu la TFF.Na kwa upande wa Simba mpa...

WAAMUZI SIMBA NA YANGA HAWA HAPA

Picha
Waamuzi Simba na Yanga hawa hapa 23 Aug 2017, 09: 0 5 am| By  TANZANIA Kuelekea pambano la ‘Ngao ya Jamii’ kati ya watani wa jadi Yanga na Simba litakalochezwa leo Jumatano uwanja wa Taifa, Dar es salaam, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetangaza waamuzi watakaochezesha pambano hilo kali na la kusisimua. Afisa habari wa TFF Alfred Lucas amewataja waamuzi hao kuwa ni Elly Sasii atakayesimama katikati, akisaidiwa na Fernand Chacha pamoja na Hellen Mduma, huku mwamuzi wa nne (4 th  Official akiwa ni Israel Mujuni Nkongo) Amesema waamuzi hao wote waliopewa jukumu la mchezo huo wana beji za FIFA kutokana na uzito wa mchezo wenyewe. Pia, Lucas amesema mechi hiyo imesogezwa mbele ambapo muda wa kuanza kwake sasa utakuwa ni saa 11:00 jioni badala ya saa 10:00 jioni iliyokuwa imepangwa awali. Takriban askari polisi 300 wakiwemo askari wa farasi watakuwepo uwanjani kuhakikisha ulinzi na usalama ambapo Lucas amewaonya wote wenye nia mbaya na wenye vurugu ...

SIMBA YAKIMATAIFA KABISA

Picha
UKIHESABU mchezaji mmoja mmoja, Simba inaweza kuwa ndiyo timu iliyosajili wachezaji maarufu na wenye uzoefu mkubwa kuliko timu nyingine za Ligi Kuu Bara msimu huu. Imeachana na wachezaji kumi na kusajili wengine 14 kutoka nje na ndani ya Tanzania. Baadhi ya mastaa waliosajiliwa ni pamoja na Mganda Emmanuel Okwi ambaye ni kipenzi cha mashabiki wa Msimbazi, John Bocco, Shomari Kapombe, Ally Shomary, Aishi Manula na Said Mohammed ‘Nduda’. “Kiujumla usajili tulioufanya ni mzuri na viongozi wamefanikiwa kuniletea aina ya wachezaji ninaowahitaji ili timu iweze kufanya vizuri msimu unaotarajiwa kuanza hivi karibuni,” anasema kocha wa timu hiyo Mcameroon Joseph Omog. “Nimepata kundi kubwa la wachezaji wazoefu, waliopevuka na wenye kiwango kizuri, ambao bila shaka watakuwa na mchango mkubwa kwa timu katika mashindano mbalimbali ambayo tutashiriki msimu ujao. “Matarajio yetu ni kufanya vizuri ambako si kwa namna nyingine bali kutwaa ubingwa kwenye kila mas...

MAGAZETI LA LEO JUMAMOSI

Picha

MKUTANO SIMBA UPO PALEPALE

Picha
SIMBA SPORTS ​ ​ DAR ES SALAAM ​ ​ 11-8-2017 ​            ​ TAARIFA KWA UMMA ​ ​ _______________________________ ​ Klabu ya Simba inawatangazia Wanachama wake na wadau wa mchezo wa kandanda kote nchini kuwa Mkutano wake mkuu wa kawaida wa kila mwaka upo pale pale. Hatua hiyo inafuatia na Hukumu iliyosomwa leo katika Mahakama ya kisutu, kufuatia zuio la kuzuia Mkutano huo, liliowekwa na mmoja wa wadhamini wa klabu Mzee Hamis kilomoni. Kwenye hukumu hiyo,mahakama hiyo ilitupilia mbali shauri hilo. Mkutano huo utafanyika siku ya Jumapili tarehe 13-8-2017, kuanzia saa Nne kamili asubuhi, ukitanguliwa kwa Wanachama wa klabu kujiandikisha kuanzia saa mbili kamili asubuhi. Klabu imeamua kufanyia mkutano huo kwenye Ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (Mwalimu Nyarere international Conference Centre). Ukumbi huo wa kisasa kabisa nchini upo maeneo ya Ocean Road, jirani na Chuo c...