Machapisho

HUYU NDO KANOUTE

Picha
​   Sadio Kanoute amekuwa ni miongoni mwa wachezaji waliozungumzwa sana baada ya mechi ya juzi dabi ya Kariakoo kati ya Simba vs Yanga, swali ni je ataendelea kutoa kile alichokitoa juzi katika mechi zijazo za Simba?. Iko hivi, uhalisia uliopo watu wengi hawamtazami Kanoute kama mchezaji mzuri anaeweza kuifanya Simba kuwa imara katika eneo la kiungo, binafsi naamini ni mchezaji mzuri ambae anahitaji muda ili kuwa bora zaidi. Kama unategemea kuona Kanoute akicheza mpira wa kukufurahisha hatakuwa mchezaji mzuri machoni mwako, yeye anatekeleza majukumu yake kimbinu na ni hapa tu ambapo watu wengi wanampa thamani ndogo kwa sababu hana mambo mengi. Ubora alioonyesha jana unaweza kuwa ni mwanzo wa kumfanya aendelee kuwa imara zaidi, kama mchezaji anaweza kucheza katika presha kubwa kama ya jana na ikapelekea azungumzwe kwa mazuri hiyo inamjenga vizuri kisaikolojia, kila la kheri kwake. #simbasctanzania #NBCPremierLeague #wingi_van_moses_ZONE

IBRAHIM AJIBU AKIONA CHA MOTO

Picha
AKIWA Rustenburg, Afrika Kusini kiungo mshambuliaji mpya wa Simba, Ibrahim Ajibu na Francis Kahata wamekiona cha moto ni baada ya Kocha Mbelgiji, Patrick Aussems kutumia saa mbili sawa na dakika 120 kuwakimbiza nyota hao. Hiyo, ikiwa ni saa chache tangu timu hiyo itue Sauzi na kuweka kambi kwenye moja ya hoteli nyota tano ya Royal Marang Hotel ya nchini huko ikijiwinda na Ligi ya Mabingwa Afrika na Ligi Kuu Bara. Ajibu alijiunga na Simba hivi karibuni akitokea Simba mara baada ya mkataba wake kumalizika wa kuichezea timu hiyo huku Kahata yeye amejiunga na timu hiyo baada ya mkataba kumalizika Gor Mahia ya nchini Kenya. Ibrahim Ajibu atakaa siku sita tu katika kambi yao ya Afrika Kusini kisha atarejea hapa na kujiunga na Taifa Stars. Meneja wa timu hiyo Patrick Rweyemamu alisema mara baada ya kutua huko juzi Jumatatu walifanya program moja ya mazoezi ya jioni kwa kutoa uchovu wa safari lakini siku iliyofuata walifanya mara mbili asubuhi na jioni. Rweyemamu alisema, programu waliyoanza...

CAF YAFANYA MABADILIKO

Picha
Shirikisho la Soka Barani Afrika CAF, limetoa mwongozo mpya kuelekea michuano ya Klabu Bingwa Afrika CAFCL msimu ujao. Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya vilabu Afrika CAF imesema kuwa katika michezo ya fainali ya Klabu Bingwa Afrika CAFCL na Kombe la Shirikisho CAFCC, utapigwa mchezo mmoja pekee badala ya michezo miwili. Pia mchezo huo mmoja utapigwa katika katika uwanja huru hauna uhusiano na timu yoyote kati ya zilizoingia fainali. Mabadiliko hayo yamekuja kufuatia kuzuka kwa sintofahamu katika mchezo wa pili wa fainali ya Klabu Bingwa Afrika msimu uliopita kati ya Wydad Casablanca na Esperance de Tunis, ambao haukumalizika kwa utaratibu licha ya Wydad kutangazwa mshindi na kukabidhiwa kombe na baadaye kupokonywa. Mwongozo huo mpya utazigusa timu wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya kimataifa, Simba SC na Yanga zitakazoshiriki Klabu Bingwa Afrika, pamoja na Azam FC na KMC ambazo zitashiriki Kombe la Shirikisho endapo zitaweza kufika hatua ya fainali.

WACHEZAJIWA SIMBA WALIOBAKI DSM KWENDA BONDENI MDA WOWOTE

Picha
Taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Simba Sc zinasema Nyota wanne wa klabu hiyo ambao waliachwa jiji Dar Es Salaam wakati wenzao wakielekea Afrika Kusini kwenye maandalizi ya msimu mpya tayari wamekamilisha masuala ya Passport zao na muda wowote watasafiri kuwafuata wachezaji wengine. . . Nyota hao ni pamoja na Meddie Kagere, Deo Kanda, Francis Kahata na Sharaf Eldin Shoboub

AZAM KANYAGA TWENDE KAGAME CUP

Picha
MABINGWA watetezi, Azam FC wamefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) leo Uwanja wa Nyamirambo mjini Kigali, Rwanda. Haukuwa ushindi mwepesi, kwani Azam FC ililazimika kutoka nyuma ili kupata tiketi ya Nusu Fainali, baada ya kutanguliwa kwa bao la Ipamy Giovanni dakika ya 21. Mshambuliaji mpya, Iddi Suleiman ‘Nado’ aliyesajiliwa kutoka Mbeya City alianza kuisawazishia Azam FC dakika ya 27 akimalizia mpira uliorudi baada ya kuokolewa kwa kichwa kufuatia mpira wa adhabu uliopigwa na Mzimbabwe, Bruce Kangwa kutoka kushoto. Wachezaji wa Azam FC wakimpongeza Obrey Chirwa baada ya kufunga bao la ushindi wa 2-1 dhidi ya TP Mazembe Na alikuwa Iddi Nado mwenyewe aliyesababisha faulo hiyo baada ya kuangushwa na Giovanni pembezoni mwa Uwanja kabla ya beki wa kimataifa wa Zimbabwe kwenda faulo iliyozaa bao lililoirejesha Azam mchezoni. Na sifa zimuendee...

MZEE KILOMONI APIGWA CHINI MSIMBAZI

Picha
Hizi ni barua zilizotoka kwa Kabidhi Wasii Mkuu wa Serikali kwenda kwa wakili wa aliyekuwa mdhamini wetu, na pia barua ya Mahakama kwenda kwa wakili huyo zinazothibitisha mdhamini huyo Mzee Hamis Kilomoni sio mdhamini tena wa klabu yetu ya Simba. Taarifa hii ilitolewa leo na Afisa Mtendaji Mkuu, Crescentius Magori kwenye mkutano wake na wanahabari.

ABDI BANDA ANOGESHA KAMBI YA SIMBA UKO BONDENI

Picha
BEKI wa zamani wa Simba ambaye kwa sasa anakipiga timu ya FC Baroka ya Afrika Kusini leo amekutana na wachezaji wa Simba pamoja na viongozi ambao wametua timu Afrika Kusini kuweka kambi. Beki huyo ameongeza furaha kwa wachezaji na viongozi wa Simba baada ya kuonana na kupiga picha ya kumbukumbu Simba imeamua kuweka kambi ya muda wa wiki mbili nchini Afrika Kusini kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao unaotarajiwa kuanza Agosti 23 na mchezo wa kwanza itamenyana na JKT Tanzania. @Wingi van moses jr.