Machapisho

OKWI NDANI YA AFRIKA KUSINI

Picha
Mshambuliaji Emmanuel Okwi, ametua katika kambi ya Simba nchini Afrika Kusini na leo asubuhi ameanza mazoezi. Okwi ameanza mazoezi na wenzake katika kambi ya timu hiyo jijini Johannesburg, Afrika Kusini.

MSUVA RASMI HASSANI EL JADIDI YA MOROCCO

Picha
Kiungo mshambuliaji wa Tanzania Simon Msuva ametambulishwa rasmi na klabu yake mpya Difaa Hassani El Jadidi ya Morocco baada ya kusaini mkataba wa miaka mitatu kuitumikia klabu hiyo. Msuva aliondoka Dar es Salaam Julai 26, 2017 kwenda Morocco ambako atakuwa na mtanzania mwingine Ramadhani Singano ‘Messi’ ambaye yeye alifika Morocco mapema kuliko Msuva aliyekuwa na majukumu kwenye timu ya taifa.

KICHUYA AHOFIA NAMBA

Picha
wakati club ya simba ikiendelea na maanadaliazi ya mchezo wa ngao ya hisani dhidi ya mahasimu zao yanga pamoja na maanadalizi ya msimu ujao uko Afrika kusini. mshambuliaji wa simba Shiza kichuya amefunguka na kusema anahisi msimu ujao itakuwa mgumu kwake kutokana na usajir mpya ndani ya kikosi chao na ujio wa emmanuel Okwi kichuya anayecheza wingi ya kulia na kushoto amesema kwa sasa simba inawachezaji wa kutosha wa kunyakua makombe na kutesa kimataifa pia kichuya anamsubiri kwa hamu okwi na niyonzima kwani anahamu ya kucheza nao kikosi cja kwanza japo anamuachia kocha ndo anajuwa nani acheze hapa au nani amalize hapa kichuya     

FLOYD MAYWEATHER TENA ULINGONI KUMUONA $150000

Picha
Tiketi za kushuhudia mpambano wa masumbwi kati ya Floyd Mayweather dhidi ya Conor McGregor zinauzwa kwa dola 150,000. Mpambano huo unatajwa kuwa wa gharama zaidi kuwahi kutokea na tiketi kwa sasa zinauzwa kama njugu. Unatarajiwa kupigwa Agosti 26 katika uwanja wa T-Mobile mjini Las Vegas utakaoingiza watu elfu 20. Mayweather mwenye miaka 40 awali alistaafu lakini amerejea kupambana na McGregor.

KITASA CHA SIMBA SPORT CLUB CHANUKIA ORLANDO PIRATES

Picha
Kampala, Uganda. Orlando Pirates ipo tayari kumnunua beki wa Uganda, Simba SC, Murushid Juuko kwa mujibu wa KickOff.com. Beki huyo wa Uganda, Juuko ameripotiwa kuwa yuko njiani kujiuanga na miamba hiyo ya Soweto, Orlando Pirates. Beki huyo mwenye miaka 23, kwa sasa yupo na kikosi cha Simba kinachojiandaa Afrika Kusini alikuwa miongoni mwa wachezaji wa Uganda Cranes walioshiriki katika Kombe la Mataifa ya Afrika 2017 nchini Gabon. Kwa mujibu wa vyanzo vya kuhaminika kutoka Uganda, Juuko alisema amekuwa akifuatiliwa na Buccaneers, ambaye wanatakiwa kununua mkataba wake wa miezi minne uliobaki na Simba. "Murushid Juuko amehusishwa na kutakiwa na Orlando Pirates,” chanzo hicho kimeimbia KickOff.com. “Ni beki mzuri anayecheza katika klabu ya Simba SC." Aliendelea kuwa: "Juuko amebakiza miezi minne katika mkataba wake wa sasa. Hivyo ni bora Simba wakakubali kuuza sasa au la kumwacha ondoke bure.”

WAZIRI JUNIOR AWAZA KUWA MFUNGAJI BORA

Picha
Mshambuliaji mpya wa Azam, Waziri Junior amesema lengo lake ni kuwa mfungaji bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu. Azam inayoendelea na maandalizi kuelekea msimu huo mpya itafungua dimba Agosti 26 kwa kucheza ugenini kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona dhidi ya wenyeji wao, Ndanda. "Inawezekana kuwa mfungaji bora wa Ligi kikubwa ni kupigania nafasi ya kuwa nacheza katika kikosi cha kwanza, changamoto ya namba ipo popote pale ila kikubwa ni kujituma. "Nimeanza kwa kufunga katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Lipuli, nafurahi kwa sababu nimekuwa na maelewano na wenzangu kwa muda mfupi." alisema. Waziri amesajiliwa na Azam akitokea Toto Africans ya Mwanza iliyoshuka daraja ili kuzipa pengo la John Bocco aliyejiunga na Simba.

DAUDA SHAFFIH AFUNGUKA KUJIENGUA KWAKE

Picha
Shaffih  Dauda anasema!! ➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖ "Unapofanya jambo lazima uangalie mwisho wake kuna manufaa gani? Nimeamua kwa maslahi mapana ya mchezo wa soka na kulinda heshima ya jina langu  kwa nia njema nimeamua kujiuzulu kugombea nafasi ya ujumbe kamati ya utendaji TFF." "Nitaendelea kushirikiana na Viongozi wa Soka kama hapo awali, kushauri na kutoa maoni yangu kama mdau katika kukuza na kuendeleza mpira wa miguu Tanzania"   "Kuonyesha uwajibikaji ni jambo Jema! Nipo kwenye mfumo wa Mpira  muda mrefu naijua mizengwe na fitna kuna watu nyuma yangu wanaonitizama ukichafuliwa kwa Rushwa ni kuharibu future yako."